Pages

Saturday 19 November 2011

Shambulio la nyuki/manyigu

Nyuki ni tisho kubwa kwa watu ambao ni lazima wafanye kazi nje: wakulima, wafanyakazi wa ujenzi, askari wa doria, na hata wacheza mpira au teseme kila mtu, Nyuki huwa wakali wanapo chokozwa na hwachagui ni nani aliye wachokoza. Nyuki aliye kasirika utamsikia sauti yake ya kuzuzizima na mara nyingi huja kichwani na usoni. Ukiwa katika hali hii jaribu kujikinga kwa kujifunika uso hasa kwa kupandisha shati lako… sorry kwa kina dada!. Vinginevyo kimbia; mwendo kasi wa nyuki unakadiriwa kuwa 19-24km kwa saa hivi ni rahisi kumshinda.
  • Usijaribu kuwapunga kwa kitabu, kitambaa au kitu chochote kufanya hivyo ni kuwapambisha moto
  • Usikimbilie ndani ya mto ziwa, bwawa au pool
  • Usijikinge uso wako kwa mikono kwani haisaidii
  • Kimbia kwa muundo wa zig-zag
  • Kama upo karibu ya nyumba au gari ingia haraka
Baada ya kurupushani hii na matokeo yake umeumwa basi fanya ifuatavyo:
  •  Ondoa ‘mkuki wa nyuki’ kwa kutumia kucha credit card au kisu
  • Usijikune
  • Jipake siki pale ulipoumwa kwa kutumia pamba au kitambaa safi ; kumbuka sumu ya nyuki ni acid kwa hiyo tumia alkaline kusawazisha sumu ya manyigu ni alikaline tumia acid kusawazisha
  • paka papai, kitunguu, kitunguu swaumu pale ulipo umwa ili kupunguza uvimbe.














No comments:

Post a Comment