Pages

Friday 18 November 2011

Hangover

Kwa kifupi pombe ni sumu. Wakati unaingiza sumu mwilini mwako, mwili utapatwa na mtiso uliosababishwa na pomba kam matokeo ya sumu hiyo kutembea mwilini mwako. Hangover ni neno mwavuli ambalo linajaribu kukueleza kitu gani umeufanyia mwili huo. Mara kwa mara dalili ni pamoja na maumivu ya kichwa uchovu, na upungufu wa maji mwilini.

OK kabla ya ‘kuyatimba maji’ zingatia:
☺ Kula hasa chakula chenye mafuta kama nyama nk
☺ Kunywa maziwa
☺ Kunywa vijiko 2 vya mafuta ya olive
☺ Meza vidonge vya vitamin
☺ Jihari usichanganye pombe


Tiba:
Dawa ya kwanza kama unafanya kazi piga simu kazini kwako na uwaambie boss kuwa unaharisha sana na kasha pata usingizi wa kutosha.
Mara tu utakapoamka pata glass mbili za maji baridi kasha kikombe kidogo cha kahawa kwa kuwa kahawa inasaidia kurudisha mishipi ya damu iliyovimba katika hali yake ya kaida jihadhari usinywe.
Kunywa juisi ya kutosha hasa juisi ya madaransi, nyanya au machungwa glasi kubwa inatosha
Jihadhari na kunywa kahawa kwa sababu caffeine siyo mzuri kwa hali hiyo
Kunywa KUDZU ni dawa ya kienyeji ya Kichina kama kifungua kinywa. Kinywaji hiki kinaweza kupatikana katika maduka ya chakula kwa afya.
Ukipata nafuu kunywa supu hasa ya kuku itasaidia kurudisha potassium uliyopoteza.
Milkshake ya ndizi; changanya nusu kikombe cha maziwa ndizi mbivu pamoja na asali vijiko vya chai 2.

No comments:

Post a Comment