Pages

Friday, 18 November 2011

Fuga Nyuki Kirahisi

Ufugaji wa nyuki ni shughuli muhimu inayosaidia jamii kujipatia mapato ya ziada ili kuboresha maisha yao.
Ufugaji wa nyuki ni mfumo wa kilimo unaohimili na wenye manufaa kwa mazingira.Ufugaji wa nyuki huwapatia watu walio ndani ya umaskini mapato ya ziada ya mara kwa mara,husaidia mazingira na huwa na manufaa mengine:
1. Ni ghali.Watu binaafsi ama mashirika ya kibinafsi kama makanisa,makundi ya wanawake,makundi ya vijanasna vyama vya mashirika vinaweza kuanza na kiasi kiodogo cha pesa.
2. Haihitaji ulishaji wa jumla wa nyuki kwani nyuki hujitafutia chakula chao kwa mwaka mzima.
3. Mizinga inaweza kutengenezwa na mafundi wa humu nchini ingawaje baadhi ya vifaa vinafaa kuagizwa kutoka ng’ambo.
4. Haihitaji ardhi,kwa hivyo wale wenye rasilmali chache wanaweza kushiriki.

Kumbuka katika mikakati ya mradi wa ufugaji wa nyuki moja ni kupata ufahamu wa uhusiano baina ya nyuki na mwanadamu katika eneo lako. Zungumza na wale wanaojihusisha na nyuki. Andamana nao wakifanya kazi na nyuki.
• Ikiwa hauna ujuzi wa kufanya kazi na nyuki,kuna uwezekano wa kujifunza mengi kutoka kwa wafugaji wa nyuki katika eneo lako.Kwa kufahamu jinsi wanavyofanya kazi,unaweza kutoa maoni ya kuboresha kwa kustahilika,na itakuwa rahisi kutumia teknolojia ya ufugaji wa nyuki inayofaa katika eneo lako.
• Pia ,unafaa kupitia visa kadhaa vya kung’atwa kabla ya kujitolea kufuga nyuki.Kung’atwa na nyuki ni sehemu muhimu katika ufugaji wa nyuki.Mfugaji wa nyuki anapaswa kukabiliana nayo.
• Pindi tu unapoelewa uhusiano baina ya nyuki wa kienyeji na mwanadamu,mawazo ya kuanzisha utaratibiu ulioboreshwa unaweza kuundwa.Yafuatwayo ni maswali yanayofaa kutiliwa maanani:
1.Ni nani wa kufanya kazi naye?
2.Vifaa gani vinafaa kutumiwa?
3.Ni wapi pa kuuza bidhaa za mzinga?

Hatua
• Ikiwa ndio unaanza ufugaji nyuki itakuwa bora ikiwa unafanya kazi na mtu mmoja ama wawili katika eneo lako.Kwa kuchagua wakulima wanaoheshimika na uhusiano mzuri na jamii ,juhudi zako zitaongezeka maradufu.Ukifuga nyuki mwenyewe na kutumia utaratibu tofauti na ule unaotumiwa katika sehemu yako
• Ni hatua katika mwelekeo unaofaa. Habari zitasambaa na punde ama baadaye utakuwa ukizungumza na marafiki ama majirani zako kuhusu ufugaji wa nyuki.
• Mara kwa mara anza ufugaji wa nyuki anza na angalau mizinga miwili. Hii itakupatia fursa kulinganisha maendeleo baina ya mizinga, la muhimu zaidi, inaruhusu mradi kuendelea ikiwa koloni moja itaangamia.
• Mabadiiliko huchukua muda. Ni lazima kuanza na wazo. Utoaji wa kufanikiwa wa wazo ni matarajio yanayoweza kutimilika ili kuanzisha utaratibu bora kwa uhusiano baina ya nyuki na binadamu katika maeneo mengine.
• Katika kupanga mradi,weka malengo yanayoweza kutimilika. Mradi mdogo,unaofaulu, una maana kuliko mkubwa uliojaribiwa na haukufaulu.
• Vifaa vitakavyotumiwa kwenye mradi hutugemea hali iliyoko.Unafaa kutathmini uwepo wa vifaa vinavyohitajika vile vile pia msaada wa kiufundi uliopo katika kuchagua aina ya ama aina za vifaa vya mzinga vinavyofaa.
• Tambua watu katika sehemu yako wanaoweza kutengeneza vifaa vya ufugaji wa nyuki ujenzi wake unaweza kuwa mafanikio kivyake.Inawza kuhitaji uvimilivu unaporatibu kupata vifaa pamoja.
• Milango ya uuzaji iliyopo kwa bidhaa za mzinga katika maeneo mengi.Tafuta watu ambao tayari wanatumia asali ama nta ya nyuki. Mara kwa maara wana hamu ya usambazaji thabiti wa bidhaa za hali ya juu. Ikiwa hawatumii asali, waoka mikate na watengenezaji wa peremende wana uwezekano wa kutoa soko.Watafute pia wale ambao wanaweza kutoa soko kwa nta ya nyuki.
Vifaa:
1. Eneo lenye miti pamoja na mauwa
2. Kitengeneza moshi
3. Mizinga iliyo na:
• Kifuniko cha juu ama paa
• Kifuniko cha ndani
• Chumba cha asali
• Chumba cha uzazi
• Ubao wa chini


A Mzinga
B Kifuniko na vile vile sega la asali litajengwa hapo





Unaweza kupata ushauri na maelezo zaidi juu ya Ufugaji na maelekezo ya wapi utapata pembejeo kupitia watu wafuatao:

- Dr. Mushtaq Osman-UDSM
- Dr. Danstan Kabialo-Afri Honey/Tanzania Honey Council
- Mr. Sosthenes Sambua-TPSF
- Mr. David Kamala-Tanzania National Beekeeping Supply Ltd
- Mr. Jumanne Msuya-MNRT Beekeeping Division

No comments:

Post a Comment