Kama kuna kitu kinacho dhalilisha mtu basi harufu ya mdomo ni namba wani.
Unaweza kupiga mswaki meno yako kwa nguvu zote, kugwangua ulimi wako, floss na kusuuza kwa mouthwash na bado pumzi yenye harufu kali anakuja kutoka nyuma ya koo lako. anaerobic bacteria wanaoishi juu ya uso wa ulimi, ndani ya mdomo na katika umio wako ni chanzo cha pumzi mbaya. Kuwepo kwa bakteria hawa kunasababishwa na kuambukizwa na sababu nyingine.
Pamoja na sababu mbali mabali zisabishwazo na tatizo hili hebu tuangalie jinsi gani unaweza kujuwa kama unatoa harufu mbaya ya mdomo? Jaribu:
1. Kuuliza wenzako kama wanahisi harufu mbaya ya mdomo wakati ukiongea
2. Kama unaogopa basi muulize wife au GF
3. Rahisi kabisa kwa wale wenye uwezo wa kunusa ramba kwenye kiwiko cha mkono(pale kiganja na mkono vinapokutana), ngoja kwa muda wa sekunde 2 kisha nusa! Unaona je? Basi hivyo ndivyo wenzako wanavyo ipata harufu yako.
Tiba:
Piga mswaki angalau mara mbili kwa siku, ni muhimu kupiga mswaki kila baada ya kula ongeza mafuta ya tee tree kwenye dawa ya mswaki au unga wa karafuu. Tumia vijiti vya meno toothpick, floosy au chelewa ya mnazi kuchokonowa meno ili kuondoa mabaki ya chakula. jaribu kukwangua ulimi kutumia mswaki au kijiko. Njia nyingine ni sukutua mdomo kila baada ya kula hii itasaidia kuondoa mabaki ya chakula.
Kuwa na kipande cha karafuu mfukoni kila uendako, uma kidogo na tafuna kila baada ya muda usikiapo kuwa ulimi ni mchachu. Jaribu kupumua kutumia mdomo, hii husaidia mdomo kuwa fresh. Tumia meno yako kusugua meno yako hii husaidia pia kufanya mdomo wako kusababisha mate ambayo yatatumika kumeza bakteria walio mdomoni. Kula machungwa mara kwa mara. Kunywa kijiko kimoja cha apple cider vinegar (siki) kabla ya kula hii inasaidi kuharakisha uyeyushaji wa chakula na kuondoa harufu mbaya.
Mwisho tengeneza chai ya karafuu; chukuwa karafuu robo kijiko cha chai changanya na vikombe 2 vya maji moto kisha sukutuwa mdomo wako mara kwa mara.
No comments:
Post a Comment